Moja ya sababu kubwa inayofanya mtu
asifanikiwe ni kukata tamaa .Mara nyingi mtu anapotafuta kitu bila mafanikio
kwa muda mrefu hukata tamaa ya kuendelea kutafuta kitu hicho na hatimaye
kushindwa kukipata kitu hicho.
Watu wengi huwa wanapenda kufikia
mafanikio makubwa lakini ni wachache wanaofanikiwa .Wengi huishia njiani kwa
sababu ya kukata tamaa.Miongoni mwa vitu vinavyosababisha tukate tamaa ya
kupata kile tunachokitaka ni :
1.Mitazamo yetu
2.Mazingira(watu wanaotuzunguka n.k)
Mambo haya yatakusaidia pale ambapo
utahisi kukata tamaa :
1.*Angalia mwisho wako* : Ukihisi kama
unakata tamaa ni muhimu kuangalia ni kitu gani utapata kama hutakata tamaa na
kama utashinda changamoto unazopitia .Angalia ni faida kubwa kiasi gani utapata
kama hutakata tamaa .Ni kama mama mjamzito anavyosubiri kuzaliwa kwa mtoto na
hivyo changamoto za kulea mimba huwa hazimsumbui.Kama ukiendelea kuangalia
mahali ulipo leo badala ya kuona utapokuwa miaka mitatu au mitano ijayo lazima
utakata tamaa.
2.*Epuka vipunguza mwendo:* Achana na
marafiki wenye mtazamo hasi na wasiotaka wewe kupiga hatua .Watu hawa ni
vipunguza mwendo ambao kila siku watakuwa wakikueleza sababu ambazo zitakufanya
usifanikiwe katika maisha yako hata kama wewe unaona unaenda kufanikiwa
.Vipunguza mwendo siyo watu wa mbali anaweza kuwa ndugu yako au rafiki yako wa
karibu .
3.*Jisemee moyoni kuwa "Hii ni kwa
leo tu "*. Brian Tracy aliwahi kusema kuwa kama unapitia changamoto kubwa
kwa siku ya leo unapaswa kujisemea maneno haya " this is just for today
" .Changamoto unazopitia leo kesho zinaweza kutokuwepo na ikawa ndo siku
ya kufanikiwa kwako .Amini kuwa kesho lazima litachomoza tena .
4.*Jua kuwa hauko peke yako* : Maisha
tunayopitia kuna watu tayari walishayapitia na hivyo unapaswa kujua wewe siyo
peke yako .Jifunze kwa waliofanikiwa na utajua kuwa changamoto unazopitia kuna
watu walipitia zaidi ya hizo unazopitia
5.*Jua kuwa Hofu Inadanganya* : Unapaswa
kujua kuwa hofu ni adui mkubwa wa mafanikio .Hupaswi kuogopa kushindwa ,Amini
una uwezo mkubwa ndani yako na hakuna chochote kinachoweza kukuzuia maana wewe
huzuiliki .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni