Wengi
tunakumbuka shairi la sungura ambalo tulipitia wakati tunasoma shule ya msingi
.Unaweza kuwa hukumbuki vizuri lakini usijali nitakukumbusha .
Mwandishi wa shairi hilo alieleza jinsi ambavyo sungura
alikuwa ameyatamani matunda na akaanza safari ya kufikia matunda yale .Akiwa
katika jitihada za kuyafikia akawa
amechoka na akatoa kisingizio kuwa ndizi zile zilikuwa mbichi na sasa alikuwa
hana haja ya kuzifikia.
Mshairi
katika shairi hilo anasema kuwa Siyo kwamba ndizi zilikuwa mbichi lakini ukweli
ni kwamba ndizi zile zilikuwa mbivu lakini Sungura alishindwa kuweka jitihada
na bidii kufikia matunda yale .Mwandishi wa shairi hilo katika baadhii ya beti
anasema :
"Karuka
tena karuka, matunda akarukia,
Mwisho
Wake akachoka, kachoka hata mk-Ia,
Penye
mti akatoka, pembeni akasogea,
Pembeni
akasogea, Subgura nakuambia.
“Sizitaki
mbichi hizi” Sungura akagumia,
“Naona
nafanya kazi, bila faida kujua”,
Yakamtoka
machozi matunda akalilia,
Matunda
akalilia, Sungura nakuambia."
Mafanikio
yako ni ndizi mbivu ambazo ukizipata utafurahi maana mafanikio ni matamu
.Kupata mafanikio siyo lele Mama inahitaji kujitoa mhanga na kujaribu bila
kuchoka .Hakuna mtu adiyetaka kufanikiwa isipokuwa tunaogopa kulipa
gharama(Paying the price ) na hata sungura alihitaji kupata ndizi zile mbivu
lakini alizikosa kwa sababu aliogopa kulipa gharama .
Kuna
mahali utafika na hakuna mtu atayekwambia kuwa sasa unakaribia kufanikiwa na
kwa kuwa hakuna mtu atakayekwambia kuwa sasa unakaribia kufanikiwa unaweza
kuacha kufanya biidii na hivyo ukaishia njiani .Haina haja ya kujichoisha kama
unajua kuwa utaishia njiani .Safari uliyoanza unahitaji kuimaliza .Mwanzishaji
wa jambo ndiye anapaswa kumaliza jambo .
Wakati
sindano inataka inatolewa mwilini huwa ndipo maaumivu yanazidi kuliko pale
inapokuwa inaingia mwilini.Wakati unakaribia kuifikia ndoto zako maumivu
yatazidi na utahisi kuacha na utataja sababu kama za sungura na maisha yatakuwa
yamekushinda na watu watakucheka ....Kwanini uchekwe??? kwanini ukate tamaa???
kwanini
Usiache
kufuata ndoto yako ,wewe ni mshindi zaidi ya mshindi ,una kila kitu cha
kukufanya ushinde , huyo anayekwambia huwezi siye aliyekuumba na hata hajui
nguvu na uwezo ulioko ndani yako .Shida hujajua wewe ni nani na unapaswa kuwa
wapi wa wakati gani na kwanini ulizaliwa wewe na si mwingine ....
Mwandishi
wa shairi la sitaki mbichi hizi anamaliza katika ubeti wa mwisho kwa kusema
yafuatayo:
"Hadithi
nimemaliza, nimekwisha simulia,
Jambo
moja sikiliza, rafiki yangu sikta,
Usikose
kujikaza, mazuri kukazania,
Utamshinda
Sungura, utapata mbivu hizi."
Joas(Jyb) 0753836463
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni