Wakati
nakaribia kumaliza Elimu fulani mahali fulani nilikuwa na kawaida ya kukaa na
marafiki tukijiuliza nini kitafuata baada ya kumaliza na kuingia mtaani.
Wengi
waliamini kuwa baada ya kumaliza wangepata kazi nzuri ambayo ingewalipa pesa
nzuri na hatimaye kupata mambo waliyodhani kuwa vipaumbele kama vile kupata
ndoa nzuri , gari ,nyumba ,mavazi,shule nzuri kwa watoto wao n,k.
Swala
ambalo wengi tumejisahahu ni kwamba tumekuwa tukifanya kazi kwa ajili ya maisha
yetu binafsi bila kuangalia kizazi tunachotengeneza kitaishije.
Je
unataka mtoto wako akimaliza abebe bahasha kama wewe ulivyofanya wakati umekuwa
kazini miaka 20+ au hata 15?
Je
unataka baada ya kustaafu ukaombe shule ya kufundisha badala ya kwenda kwenye
kampuni yako ?
Ndugu
zangu ipo haja ya kugeuza fikra zetu za kufanya mambo kwa ajili ya mambo ya
muda tu bila kuangalia maisha baada ya kuzeeka,kustaafu ,kuachishwa kazi n.k.
Mwandishi
mmoja anasema kuwa binadamu ni kama digidigi au simba .Anaeleza kuwa wakati
simba anamfukuzia digidigi mara nyingi digidigi hushinda mbio hizo ili asiwe
kitoweo cha simba .Lakini simba huwa hajiumizi sana kukimbia maana anajua
atapata kitoweo kingine.Swali ni je kama digidigi akisimama atapona?.Jibu ni
hapana.
Mwandishi huyo anafafanua mfano huo kuwa :
- Kama ikitokea ukaachishwa kazi leo maisha yako yakayumba basi wewe ni digidigi
- Kama ukistaafu leo maisha yako na familia yako ikayumba wewe ni digidigi
- Kama ukaumwa leo usirudi kazini maisha yako yakayumba basi wewe ni digidigi ambaye mara asimamapo tu wakati anafukuzwa na simba huwa kitoweo
Wewe
ni shahidi hapo mtaani kwako:
- Yule ndugu aliyestaafu unajua maisha yake yalivomagumu kama vile hakuwa kufanya kazi
- Yule ndugu alivyopata matatizo na akashindwa kurudi kazini unajua maisha yake yalivyo ya shida
FANYA
KAZI KWA AJILI YA VIZAZI NA VIZAZI SIYO TUMBO LAKO TU.
USIPOKUWAMAKINI KESHO UTACHEKWA
Joas(Jyb)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni