NAMNA YA KUISHI MAISHA YENYE
MAANA
Utangulizi .
Watu wengi hudhani kuwa maisha ni uwezo
wa kupata mahitaji yake binafsi (Kupata
gari,mke au mume mzuri ,fedha,kula
vizuri n.k)
Wapo watu wanaoamini kuwa maisha ni
kusoma ,kufaulu na baadae kuja kuajiriwa na kuwa mtu mkubwa sana na mtu mwenye
heshima mtaani .
Nilivyokuwa chuo kikuu mahali fulani
niliwasikia vijana wakisema kuwa maisha yatakuwa yamekamilika pale
watakavyomaliza na kupata pesa nyingi zitakazowawezesha kupata kila
wanachokitaka (mke au mume mzuri ,gari ,starehe n,k).
Jamii huamini mtu asiye na fedha ,cheo
,umaarufu , shule huyo hana maisha na
mtu huyu hudharaaulika na yeye mwenyewe hufika mahali anakata tamaa na kuona
kama amezaliwa wa bahati mbaya na hana maisha .
Ukweli ni kuwa kuwa na fedha ,vyeo na
kila kitu hakuwezi kusababisha kuwa na maisha yenye maana.
Maisha yenye maana ni nini basi?????
je ni kupata mke/mume mzuri na kuwalingishia wenzako????
je ni kupata elimu nzuri ????
je ni kupata mali na kila kitu ????
maisha yenye maana ni haya hapa
Kujua Kusudi la kuja HAPA duniani
.hujalijua kusudi hujaanza kuishi
kanuni ya kuishi maishi yenye maana ni
hii hapa
Thamani yako(your values)+Uwezo
wako(your core strength)+Kiu yako(Your Passion)+ huduma yako(your service )=Kusudi
lako=maisha yenye maana
Ili uishi maisha yenye maana lazima
ufuate kanuni hiyo vinginevyo maisha yako hayataleta maana yoyote hapa duiani
haijalishi utakuwa na vingapi vinaavyoonekana .
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni