Emanuel
Mgogo mwimbaji wa nyimbo za Injili katika moja ya wimbo ulio katika albamu yake
mpya anasema " siku moja alikuwa anasafiri kutoka sehemu moja kwenda
nyingine kwa basi na wakati wanakaribia kufika mwisho ,ghafla ajali ikatokea na
watu wengi walipoteza maisha ila yeye alifanikiwa kuokoka katika ajali mbaya
ile?"
Inasikitisha
sana na inahuzunisha mno watu wamesafiri kutoka mbali na wakati wanapokaribia
kituoni na wakiwa na furaha ajali inatokea .Huwa ni vilio vikubwa sana na mara
nyiingi watu huweza hata kujiuliuliza kwanini ajali ile inatokea mwisho wa
safari na siyo vinginevyo japo ajali haipangwi na haipangiwi.
Maisha
yetu ni kama safari ya basi inayotoka sehemu "A" kwenda Sehemu
"B".Wakati mtu anataka kufika sehemu B kuna vitu vingi anapitia
.Atakutana na vituo ambavyo atasimama kwa muda mfupi na vituo atakavyosimama
muda mrefu ili kupata nguvu za kusonga mbele .
Wakati
unaendelea na safari ya maisha yako ,kama vile gari linavoweza kupata pancha na
mengineyo hata wewe pia katika safari ya maisha yako yapo mengi yanayotokea
ambayo yanapaswa kutozuia safari yako .
Jambo
moja ambalo linauma ni pale ambapo ulikuwa unataka kufikia ndoto zako ghafla
ukaacha ndoto zako kwa sababu yoyote ile.Hii ni hatari sana inaumiza sana .Ni sawa na mama mjamzito
aliyebeba mimba kwa miezi tisa akavumilia lakini akashindwa kuvumilia maumivu
ya mwishoni.
Tumekuwa
na ndoto nyingi na mambo mengi amabayo tunanafanya /kuanzisha lakini
tuavyokaribia kufika mwisho ghafla mambo ya ajabu yanaingilia ili usifike
mwisho na mara nyingi mwisho ndo unaangaliwa sana .Jana katiika Moning Rise Up
nikwambia kuwa unapaswa kuangalia mwisho kuliko mwanzo .Jitahidi sana
kutopotelea mwisho ili ndoto zako ziwe kweli.
Joas(Jyb)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni