MCHAWI ALIYEIROGA TANZANIA (SEHEMU YA KWANZA)
KUTOJIAMINI SISI
WENYEWE
Kuna
kituko ambacho kimebeba umaarufu sana kwenye jamii yetu kwa sasa, kinasema;
“maprofesa
walikuwa wakisafiri kutoka eneo moja kwenda eneo jingine, wakawa wamepanda
ndege ya pamoja kwa ajili ya kuondoka, muda mchache kabla ya ndege ile kupaa
akaja mhudumu na kuwaweka sawa kwa ajili ya safari na kuwakaribisha katika
ndege ambayo imetengenezwa na mhandisi aliyemaliza chuo kikuu UDSM, wale
maprofesa wote walikuwa wanatokea chuo hiko waliposikia tu kuwa ndege inayotaka
kupaa imetengenezwa na mwanafunzi waliomfundisha wakaamua kushuka na ndani ya
ndege alibaki profesa onyango. Walipomuuliza mbona anabaki hashuki katika ile
ndege akawajibu kuwa kama ni mwanafunzi aliyemfundisha yeye hiyo ndege haiwezi
kupaa”
Wale
maprofesa wengine waliogopa kubaki mule ndani kwa kuwa waliogopa kuwa ile ndege
ni lazima itaanguka tu na aliyebaki alikuwa anaamini kuwa haiwezi kupaa kabisa.
Watanzania
wengi sana hatujiamini kuwa tunaweza tukafanya mambo sisi wenyewe na yakawa
bora zaidi ila tunachokiamini mar azote kuwa vitu ili viwe vizuri ni lazima
vifanywe na watu wa ngozi nyeupe. Hata kuwe na mkataba wa kufanya huwa ni ngumu
sana kwa waafrika kuaminiana kuwa wanaweza kufanya ila ni rahisi kuamini kuwa
shughuli kama hizo ili ziwe bora ni lazima zifanywe na wazungu.
Tunavyuo
vingi sana vinavyozalisha wahandisi wa fani mbalimbali ila huwa hatuwaamini na
kuwatumia kuwapa kazi badala yake kazi zetu tunaenda kuwapa wakandarasi wa
kutoka nchi za nje kama china, marekani na ujerumani. Ukiangalia sana utagundua
kuwa hatuwaamini wakandarasi ambao wanazalishwa kila mwaka na vyuo vyetu na
hata wao imewapelekea kutojiamini na hata wakisoma wanaishia kuwaza kuwa
wakandarasi wa kujenga nyumba na kusimamia mabomba ya maji na hawawazi kabisa
kama wanaweza kupewa nafasi ya kusimamia mambo makubwa.
Kama
wakandarasi wa kutoka nje ya nchi zetu wanaweza inashindikana vipi kwa
wakandarasi wa ndani ya nchi kushindwa. Ni lazima tuanze kuwajengea uwezo wa
kujiamini kuwa wanaweza kufanya mambo makubwa. Kama tutawaamini na kuanza
kuwaachia wafanye wataishi kwa kujiamini na kujipa wajibu wa kugundua mambo
mengi zaidi sana.
Kwa
mfano kwa sasa Tanzania tunatembea katika kauli mbiu inayoamini katika kuifanya
Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Swali la kujioji ni, hii nchi ya viwanda
itajengwa na wakandarasi kutoka nje ya nchi au wa humu ndani ya nchi. Umefika
wakati ambao lazima tukiamini tulichonacho na tuanze kukitumia.
Mbali
na masuala ya kiuandisi ukienda katika eneo la afya bado utakuta tatizo ni lile
lile. Hivi kama India na Marekani wangekuwa wakiumwa wanawaleta watu wao kuja
kutibiwa Afrika ni lini wangetengeneza wataalamu wao wenyewe ambao wangekuwa
madaktari bingwa ambao leo hii wamekuwa kimbilio. Au madaktari wan chi kama
hizo wanavuta pumzi tofauti na madaktari wa huku kwetu, au wanawazidi kitu gani
haswa. Ni kweli kuna sehemu lazima tutakuwa tunazidiwa nao haswa katika eneo la
ujuzi, ila tunafanya kitu gani ili kuondoa huo mwanya. Ni lazima tujikite
kuwekeza katika madaktari wetu na kufanya namna yoyote ile itakayowasaidia kuwa
wagunduzi zaidi.
Ukimsoma
Daktari maarufu sana Ben Carson aliyetenganisha mapacha walioungana vichwa
utagundua kuwa aliwekeza zaidi katika kufanya utafiti ambao leo hii umemfanya
kuwa Daktari maarufu zaidi. Bado naamini inawezekana na sisi tukapata wataalamu
zaidi ya Ben Carson kama tutawekeza zaidi katika kujiamini sisi wenyewe zaidi
ya kuamini kuwa wazungu tu ndio wanauwezo wa kufanya mambo makubwa kama hayo.
Mara
nyingi tumekuwa tukishuhudia wakiibuka vijana wanaogundua vitu vya
kiteknolojia, kuna mwingine alitengeneza ndege kabisa, kuna wengine walianzisha
vituo vya redio kwa kuunga unga mitambo na ikafanya kazi kama vituo vya redio
za kawaida. Pamoja na vitu kama hivyo hawa watu wamekuwa wakiishia kutosikika
tena na hakuna anayethamini juhudi zetu kwa sababu hata viongozi wetu hatuamini
sana kama wanaweza wakafanya vitu vikubwa. Nchi zinazofanya mapinduzi ya
viwanda haziwezi kuacha kupuuza kuwa na watu kama hawa na kuwapatia nyenzo muhimu
zaidi wanazozihitaji ili wafanye makuu zaidi.
Rafiki
yangu Mabula Jilala wakati akiwa anasoma sekondari kama kidato cha tatu alikuwa
na mawazo ya kuja kuwa mhandisi na atengeneze Trekta kwa kuwa alichoshwa na
mahangaiko ya kilimo cha jembe la mkono. Na alikuwa akijaribu kufanya hivyo na
alianza kuchokonoa injini ya Trekta bila kufundishwa na mtu yeyote na
akafanikiwa kuwasha Trekta ilo, ila hakukuwa na mtu wa kutazama juhudi zile na
hata watu waliokuwa wakimuona walimtazama kama kijana mtundu tu, na sasa haendelei
na ujuzi huo tena.
Tunao
wataalamu wengi sana katika jamii yetu kama tutakuwa makini kuwatumia itasaidia
kweli kuwa nchi ya mapinduzi ya viwanda.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni