NAMNA YA KUTUMIA BUTI LA GARI LAKO KIBIASHARA??
Leo nitakuueleza namna
ambayo buti La gari lako Unaweza tumia Kama duka na ukawa unaingiza
fedha. Watu wengi wamekuwa wakitumia buti la gari katika Kubeba vitu ambavyo si
vya kibiashara.
Unaweza kununua vitenge
, Viatu, n. K ukawa unasambaza maofisini na kila unapokutana na marafiki zako.
Kuna wakati unakutana na
watu muhimu Ni vizuri ukawa na bidhaa kwenye gari. Beba Juice ya matunda na
wauzie wafanyakazi. Beba viungo, bidhaaa za makampuni yanayofanya kazi kwa
mtandao Kama Umejiunga n. K.
Mara nyingi tumekutana
na watu wengi katika matukio mengi na tumekosa fursa kwa uzembe wetu.
Leo Fikiria namna ya
kufanya buti lako liwe kiuzalishaji zaidi.
KWA MAWAZO YA KIBIASHARA NITAFUTE WATSAP 0753836463
"MAMA HUYU HUPATA MILIONI MOJA NA NUSU KWA MWEZI AKIUZA CHAPATI MIA KILA SIKU"
Akili yako ndo utajiri wako au umaskini
wako !
Mama mmoja ambaye hakutaka jina
lifahamike aliamua kuanza kutengeneza chapati na kuziuza eneo la Posta (watu
husema mjini).
Mama huyu hutengeneza wastani wa chapati
mia moja kila siku na kuzisambaza maofisini ambapo kila chapati huuzwa sh 500
/=.kwa hiyo akiuza chapati zake zote 100 hupata sh elfu hamsini kwa siku na kwa
mwezi hupata milioni moja na nusu .

Huamka asubuhi na mapema kuwahi watu
wanaotafuta vitafunwa maofisini ,kama unavojua Watnzania ni wavivu wanapenda
vya kuletewa .Sasa uvivu wako ni fursa kwa mwingine .
Mama humaliza kuuza chapati majira ya sa
nne asubuhi na hurudi nyumbani kwake kuendeleza genge .Mbali na chapati huuza
pia mihogo,sambusa n,k maofisini na zingine huacha kwake .Mama huyu hutengeneza
kipato kikubwa sana kwa siku na kwa mwezi hukusanya zaidi ya milioni mbili.
Endelea kuamini unachokiamini huku
ukiendelea kuwa maskini jeuri .Chapati ni zaidi ya mishahara yako ya miezi
mitatu.Kwanini usiuze chapati ??????????
Usikose makala za fursa na ujasiriamali
kila alhamis
Kamata fursa .
Joas(Jyb) Watsap 0753836463
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni