Leo
nataka kugusia jinsi rubani wa ndege anavyopotezwa na waongozaji wa ndege (Air
Traffic Controllers) .
Waongozaji
wa ndege ni wataalamu wa mambo ya anga na hukaa kwenye chumba maalumu
wakiwasiliana na Rubani juu ya usalama wa Anga na hali ya hewa ya anga ili
kumsaidia Rubani kuweza kuifikisha ndege salama.
Ni
wazi kuwa kama Muongoza ndege hatawasiliana vizuri na Rubani na kumpa taarifa
sahihi za anga ,kuna uwezekano ndege ikapata shida njiani.Hivyo umakini wa
muongoza ndege na mawasiliano mazuri na Rubani huifikisha ndege salama .
Ndugu
,unaweza kuona sasa jinsi ambavyo Muongoza ndege ana mchango mkubwa katika
kuhakikisha ndege inafika salama au isifike salama.
Ajali
nyingi ulizowahi kusikia ni makosa ya mawasiliano na taarifa za anga ambazo si
sahihi kutoka kwa waongoza ndege.
Unapaswa
kujua kuwa kwenye maisha yetu ya kila siku kuwa wewe ndo rubani wa ndege yako inayokupeleka
kwenye uwanja wa mafanikio na wapo wanaoogoza ndege yako au wanataka kuongoza
ndege yako ya Mafanikio unapaswa kuwa nao makini maana wanaweza sababisha
kufika au kutokufika.
Watu
wenye kiu ya kutaka wewe ufanikiwe,wanaokuonesha mbinu za kufanikiwa , wanaokushauri
n,k hawa ni waongozaji wazuri na watakufikisha mahali unapokwenda japo
changamoto njiani utazipitia.
Wapo
wale waongozaji wengine ambao ni waongozaji wabaya ambao hawataki wewe
ufanikiwe na mara nyingi ni watu wa kukukatisha tamaa na kukuvunja moyo hawa
una kila sababu za kutowasikiliza maana ndege yako ya mafanikio haitafika.
Leo
una maamuzi ya kuchagua nani anapaswa kuwa Muongozaji wa ndege yako ya
mafanikio ambaye atahakikisha ndege yako kufika
inakokwenda kinyume na hapo utaishia njiani .
Joas(Jyb)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni