Ijumaa, Julai 29, 2016

"Je,umepandwa mahali sahihi?"




Kuna wakati fulani kwenye kundi la kijana Jithamini watsap (Waweza kujiunga kwa kutuma namba yako hapa 0753836463) niliwahi uliza swali hili "Mkulima A alipanda mbegu katika  shamba B  lakini mara kadhaa mkulima huyu alikuwa havuni kwa miaka mingi sasa .Nini unaweza mshauri ?"

Watu kadhaa waliweza kuchangia nini zinaweza kuwa sababu za kukokosa mavuno na haya yalikuwa baadhi ya majibu :

Christina moja ya manachama wa kijana jithamini anasema "nitamshauri asikate tamaa ajaribu tena coz mjasiriamali ni risk taker kwa habari ya kilimo inawezekana alifuata hatua zote na eneo lina tutuba ya kutosha ila mvua ikanyesha zaidi  kama mwaka huu au ikawa pungufu "

Mabula Jilala mwamdishi na mmiliki wa Morning Tanzania blog anasema"kama mvua zilinyesha kuna mambo kadhaa huenda yalisababisha :
 1. Mvua ilizidi sana ikayaharibu
 2.Udongo haukuwa na rutuba au ulikuwa haufai kwa mbegu hizo
3.Hakutumia wadudu waharibuo mazao ya mahindi "

Abdulnuru mwanachama wa kijana jithamini anasema"awe anafanya reseach kabla hajaanza kulima coz sio mazao yote yanakubali kila mazao "

Majibu yote yalikuwa mazuri na yanaweza kuwa sababu ya mkulima kushindwa kuvuna (kupata mazao).Mfano huu una maana kubwa katika maisha .

Mkulima hapa anafananishwa na mwajiri na mbegu ni mwajiriwa na shamba linafanishwa na kampuni/taasisi ambayo mwajiriwa huyu kaajiriwa.Ukweli ni kwamba unapoajiriwa kwenye kampuni au taasisi yoyote umepandwa na sasa kama wewe umepandwa kampuni tunategemea tuone mavuno(maisha yabadilike).

Kuna mtu anakaa miaka 10 hadi 15 kwenye kampuni maisha hayabadilii(hakuna mavuno) hii inamanisha umepandwa katika shamba ambalo silo .Hata kama unapata mshahara maisha hayabadiliki,akili imedumaa na mawazo yamekwazuliwa,huna amani wala furaha .Tatizo hapo ni kuwa umekosea shamba na unapaswa kutafuta shamba mbadala ili uvune . shamba lako mbadala labda ni Kipaji kinachoweza kuutajirisha au hata viinginevyo .Wakati mwingine mbegu zinakuwa nzuri lakini shamba likikosewa hakuna kitakachovunwa .

Ushauri wangu ni kuwa ni muhimu sana kufanya tathimini ya nini kimeongezeka maishani mwako wakati ukifanya kazi katika kampuni A au taasisi.Maisha ni mafupi sana yatupasa  tuanze kuona mavuno yenye tija.

Joas(Jyb)





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni