Moja ya sababu zinazofanya kuwepo kwa
kundi kubwa la watu ambao hawana ajira ni imani zilizojengekeka juu ya elimu za
darasani ambazo hulenga kutoa vyeti badala ya kumtengeneza mwanafunzi kupambana
na mazingira.Uliwahi kujiuliza kama tungekuwa tunasoma bila vyeti ungeishije?
Ukweli ni kwamba wakati nasoma sikuwa
naamini kuwa mtu mwenye shahada ya pili (Master degree ) anaweza kosa
kazi.Lakini ukweli ni kwamba kuna watu wengi wenye shahada ya pili na hawana
kazi.(Shida ni nini?)
Shida ni kwamba vyeti tunavyopata vinatufanya tutengeneze matabaka
na kuwa na makundi kadha wa kadha japo hatuna uwezo sawa na vyeti tulivyonavyo
.Nakumbuka wakati nasoma shahada ya Kwanza chuo kikuu cha Dar es salaam sehemu
ya mlimani kulikuwa na matabaka ya kozi tunazosoma .
Wakati huo Mtu anayesoma uhandisi
alijiona bora kuliko mtu anayesoma kozi yoyote ile lakini ukweli ni kwamba huyu
mtu wa uhandisi akiingia mtaani anaanza
kuhangaika kutafuta kazi maana elimu
aliyonayo ni nadharia na hawezi kuonesha
ubunifu wa kihandisi.
Ni elimu za vyeti zimetufanya tuchague
kazi za kufanya hata kama mtu hana kazi
yoyote kwa muda huo .Nani aliyekwambia mtu mwenye shahada hawezi uza chips?
.Elimu zetu zitusaidie kufanya vitu wanavyofanya watu wengine lakini kwa ubora zaidi .
Ushauri wangu ni kuwa pamoja na kwamba
tunaenda shule ni vizuri tukayatafuta maarifa .Maarifa ndo yanayotufanya tuishi
hata kama mazingira hayawezi kupokea vyeti tulivyonavyo.wewe ni shahidi kuna
walimu wamemaliza toka mwezi wa saba mwaka jana na mpaka sasa
hawajaajiriwa.Ukifanya utafiti wa kujua nani anajihusisha na chochote kabla
hajapata hiyo ajira ni wachache sana .Wengi wanalaumu tu kuwa serikali
imechelewesha ajira badala ya kutumia eimu aliyopata .
Elimu bila Maarifa haitakusaidia :
- Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.(BIBLE)
- Na kwa maarifa vyumba vyake hujazwa Vitu vyote vya thamani na vya kupendeza.(BIBLE)
- Mtu mwenye hekima ana nguvu; Naam, mtu wa maarifa huongeza uweo(BIBLE)
- Wajinga hurithi upumbavu; Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa .(BIBLE)
Joas 0753836463
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni