Jumatatu, Julai 18, 2016

ONA MAAJABU HAYA ~Joas Yunus


Asubuhi hii nikiwa kwenye gari , nikiwa natafakari Juma lilinavyoanza ghafla nikaanza kuwaza maajabu haya ya dunia .Ndiyo kwangu mimi ni maajabu japo wewe unaweza kuona kawaida .

Starter ambayo wenzangu na mimi wanasema “stata” ni kitu cha ajabu sana .Kwa wasiofahamu starter huwa kwenye magari ,pikipiki ,tubelights n.k. starter ndo husaidia uanzaji wa gari na vifaa vinavofanana na hivyo.Usione magari makubwa na mazuri yanapita barabarani bila starter hayawezi kwenda kuwaka na kwenda kokote .

Nilipokuwa nasoma masomo yangu ya Olevel ,madarasani tulikuwa tunatumia tubelights .Wakati wa maandalizi (Prepo) wale wanafunzi wasiotaka kujisomea na wavivu walikuwa wanapenda kuchomoa starter kwenye tubelights hizo na wakishachomoa tubelights zilikuwa zinashindwa kuwaka.Wanafunzi hawa wazembe wa kujisomea Walijua fika bila starter wale ambao walikuwa wanasoma kama wametumwa na vijiji vyao wasingeweza kujisomea .

Anyway nisiongelee sana stori lakini point yangu hapa ni kwamba maisha yako yako kwenye kuanza .Unahitaji sana starter yako mwenyewe(self-starter) ili ufike unapotaka kwenda .Ukiona mtu hafanyi kile alichopanga kufanya ujue huyo starter yake imechomolewa .

Siri ya watu waliofanikiwa walikuwa na uwezo wa kuanza vitu maana walikuwa wana starter zao wenyewe na walipogundua kuna watu wanataka kuficha starter zao walikuwa makini sana na leo wamefika mbali .

Jana Rafiki yangu Lameck Amos Hulilo muhitimu wa masomo ya uhandisi wa chuo kikuu cha Dar es salaam katika masomo ya uhandisi wa tarakirishi (computer) mwaka 2014 ambaye ni mkurugenzi wa Kampuni ya Mpango Mkakati Technologies iliyoko eneo la Ubungo Dar es salaam alitueleza kwenye kundi la Kijana Jithamini kuwa pamoja na kwamba sasa anamiliki Kampuni yake binafsi lakini ameanza huduma ya kutoa chakula  ambayo yeye ameiita kwa jina la EAT & SAVE (Kula na uokoe pesa).Lameck ni mtu mwenye nguvu kubwa ya kufanya maamuzi yake mwenyewe katika kuanza jambo (self-starter) .Big up kwake .

Mpendwa bila kuwa na nguvu ya kuanza jambo hutafanya lolote katika na maisha yako na utakufa ukiwa umewaachia mzigo wanaobaki kwa mipango yako mingi iliyoandikwa kwenye makaratasi .Nani kakwambia ili uanze unahitaji kuwa na milioni moja??? Nani kakwambia ili uanze unahitaji kuwa mtu maarufu ??? .Hee hujui Huyu Lameck alianza kutengeneza Business card za watu??? .Come on unajua hapo ulipoajiriwa huyo mkurugenzi alianza na mtaji kiasi gani??? .Shida siyo mtaji shida ni kukosa starter yako mwenyewe .

Jyb (0753836463/0656110906)




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni