Jumatano, Julai 13, 2016

“MTI UKIKATWA HUWA UNACHIPUKA TENA “




Huwa nashangaa jinsi ambavyo mara zote mti ukikatwa huwa unachipuka tena .Hata hivyo napata jibu kuwa mti siyo matawi lakini ni mbegu iliyopandwa chini na ikatengeneza mizizi ambapo mizizi hiyo isipong'olewa mti lazima utaota tena hata kama ukikatwa.

Naamini hata wewe uliwahi kukata mti na ukadhani kuwa hautaweza kumea tena na ukashangaa kuona kuwa mti umechipua tena kwa uzuri na kwa kustawi kabisa pengine kuzidi hapo awali .

Kuna wakati pengine watu walitaka /wanataka kukatisha ndoto zako na maono yako ili usifikie mahali Mungu amekutakia kufika ,watu hawawezi kukatisha ndoto zako maana Mungu alishawekwa mizizi ya kufanikiwa kwako na hakuna namna utakavoshindwa kuchipuka tena na kufikia hatma ya maisha yako .

Kuna watu wanaotamani upitie kwenye changamoto kubwa na uannguke vibaya ili wakucheke lakini ninachoamini n kuwa haijalishi utaanguka mara ngapi lazima usimame tena maana unao uwezo na nguvu za kuinuka na Kusonga Mbele .

Nguvu yako haiko kwenye vitu vinavyoonekana na unavyomiliki (matawi) ,nguvu yako na uwezo wako viko ndani yako na hakuna mtu mwenye uwezo wa kuviondoa mpaka hapo utakapoamua mwenyewe na huo ndo utakuwa mwisho wa ndoto zako .

Ukweli ni huu kwamba watu wengi wanatamani usifanikiwe na kusonga mbele na wamejiandaa na mapanga yao ili ukkatwe.Mapanga yao ni maneno ya kukatisha tamaa,vikwazo  n,k .Hata hivyo hawataweza kama unajua uwezo ulio nao ambao ndio unakupa uwezo wa kusonga mbele na kuendelea kufanya.


0753836463/0656110906

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni