Ijumaa, Julai 15, 2016

"JUA SABABU KUBWA YA KUTOFANIKIWA KWAKO" ~Joas Yunus

Moja ya tofauti kubwa kati ya watu Maskini na matajiri  ni juu ya matumizi ya muda .Maskini hana nidhamu katika matumizi ya muda na hivyo hudhani kuwa muda alionao utaendelea kuwepo  na hivyo huutumia vibaya wakati huo tajiri hutumia vizuri kila sekunde anayoipata .

Ukiwauliza watu waliofeli kwenye mitihani ya kidato cha sita yaliyotangazwa jana kujua kipi kimepelekea wao kufeli ,wengi watakueleza kuwa Muda wa kidato cha tano na cha sita ni mdogo sana na mambo ni mengi .Hii ndiyo tabia ya mtu anayeshindwa na maskini ambaye kila siku huleta visingizio .


Kwa upande Mwingine ukiwauliza watu ambao wamefaulu sana katika matokeo atakwambia kuwa moja kati ya vitu ambavyo vimepelekea wao kufaulu vizuri ni kuwa walitumia muda vizuri baada ya kuona kuwa vitu ni vingi na na hivyo kutumia muda mwingi katika kujisomea .

Ukichunguza na kupata ukweli kwanini watu wengi ni maskini ,utangundua kuwa maskini  hutumia muda mwingi sana kwenye starehe ,mapumziko hata kama hajafanya kazi, kupiga stori na kuwaongelea watu wengine(umbea) .Maskini hutumia muda mwingi kulaumu wengine huku wasijue kuwa wanapoteza muda.Kumbuka hao unawaoongelea wanafanya yao ya kujenga maisha  yao 

Matajiri huwa ni watu ambao hutumia muda katika mambo yenye tija .Huwekeza sana muda wao kupata maarifa (kusoma vitabu ,kuangalia video zenye kuwaendeleza n.k).Matajiri hufuata ratiba zao walizojiwekea  na siyo bendera kufuata upepo .

Mungu alitoa masaa 24 kwa kila mtu ,shida inakuja kwetu kwa namna tunavyotumia muda .Muda huwa siku zote unatosha isipokuwa wengi tunakosa uelekeo na kufanya yale ambayo hatukupanga kufanya .Tumekuwa watu wa kuyumbishwa na ratiba zetu wenyewe na tumekuwa bendera fuata upepo .

Utawezaje kutumia muda wako vizuri??

1.Andika vitu utakavyofanya kesho kabla hujaenda kulala
Kutojua kesho utafanya nini ni hatari sana na ndio sababu kubwa inayopelekea unapoteza muda mwingi kwa kufanya mambo yasiyo na tija .Ni muhimu sana kama unataka kufanikiwa uwe na tabia ya kuandika yale yote ambayo utafanya vinginevyo utafanya lolote na kukuta kuwa siku imeisha bila kufanya mambo ya msingi .

2.Weka vipaumbele
Ni muhimu baada ya kuandika utafanya nini kujua vipaumbele vyako ni vipi kwa siku hiyo.Mambo yote uliyoyaandika yanaweza yakawa siyo yote ya msingi  .Unashauriwa kuanza kufanya yale ambayo  ni ya muhimu sana .Hii inakusaidia kumaliza mambo yote ya muhimu kwa siku hiyo .

3.Weka Nidhamu kwa uliyoyapanga
Kuandika utakachokifanya inaweza kuwa rahisi sana lakini shida kubwa iko kwenye kufuata kile ulichokiandika.Hakikisha unajenga nidhamu kubwa juu ya mambo ulijiwekea mwenyewe .Acha kabisa kufuata ratiba za watu wengine .Fuata mambo yako.

Ndugu huwezi jua thamani ya kitu mpaka pale utakapokipoteza na kutoweza kukipata tena .Muda huwa hauwezi kujirudia (Time is non renewable resource).Watu wamejikuta wakijuta kuwa kama wangelijua wangelitumia muda vizuri .Siamini kama hawa wanaojuta hawakujua kuwa muda ni Mali .Amka sasa jiwekee utaratibu mzuri wa kutumia muda(time management).

Jyb (0753836463/0656110906)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni