Waswahili husema majuto ni mjukuu
wakimanisha kuwa mtu hujuta baada ya kupata hasara .Watu wengi sasa wameishi
maisha ya kujuta na hawana tumaini la maisha yao .
- watu wanajuta kusoma chuo fulani
- watu wanajuta kusomea masomo fulani
- watu wanajuta kuolewa au kuoa mtu fulani
- watu wanajuta kwa maamuzi ambayo waliwahi kufanya. n.k

Nakutana na watu ambao wanajuta ati
kwanini hawajaenda shule wakati huo wao ndo walikuwa sababu ya kutokwenda shule
kwa makusudi na sasa wanajuta Wamesahau kuwa maisha ya binadamu hayajirudii na
daima tupatapo nafasi ya kufanya jambo tunapaswa kulifanya tukijua kuwa nafasi
hii haitajirudia tena (life is irrevisible)
Kujuta ni matokeo ya maamuzi ambayo
tulidhani ni sahihi hapo awali lakini baadae tukagundua kuwa maamuzi yale
yalikuwa si sahihi na sasa hakuna namna tena ya kufanya .Kama hii ndo sababu
ipo haja sasa ya kuwa na umakini wa kila tunaloifanya katika maisha yetu na
maamuzi ya kila siku ambayo tunafanya .
Kuna watu hujuta baada ya kustaafu kazi
na kuona kuwa na kujikuta kuwa hajafanya
chochote juu ya hatma ya familia yake ilihali alikuwa na nafasi kubwa ya
kufanya vitu vikubwa wakati bado hajasataafu .Huu ni Ugonjwa ambao umewaathiri
watu wengi sana na unapaswa kuwa makini sana wewe unayesoma
makala hii.
Kuna watu wamezungukwa na fursa nyingi
na wanashindwa kuzitumia huku wakidahani kuwa kila siku fursa zitakuwepo na
wamesahau msemo ule unaosema kuwa opportunity never come twice (nafasii haiji
mara mbili).Siku wakistuka na kutaka kufanya mambo wanakuta fursa ile haipo
tena na wananza kujuta .
Ushauri wangu ni kuwa ni vizuri kutumia
kila fursa unayokutana nayo maana wewe usipoitumia fursa yupo mtu atakayeitumia
na utajuta kwanini hukuitumia fursa ile kwa wakati ule .
Kuna watu wana nafasi ya kufanya vitu
vikubwa na mawazo makubwa lakini kwa makusudi hawafanyi chochote na kuweka
mawazo yao kwenye utendaji na utawasikia wakisema watafanya kesho,keshokutwa ,mwakani utafikiri
yaliyoko mbele wanayajua .Ndugu amka nafasi ni hii usije ukajuta.Nani kakwambia
kesho utakuwa na nguvu kama ulizo nazo leo????
Ukweli ni kwamba sisi ndio wasababishaji
wa majuto katika maisha yetu .Tumekuwa watu wakupuuzia vitu vidogo na kufanya
maamuzi yasiyo sahihi tusijue kuwa yana madhara makubwa .Kuna umuhimu sasa wa
kuanya mambo kwa uangalifu mkubwa kuepuka majuto.
Jyb(0753836463/0656110906)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni