Alhamisi, Julai 21, 2016

HUU NDO UHURU ULIOCHELEWA ~Joas Yunus



Wote  tunajua maana ya uhuru .Na kama hujui tutasaidiana hapa chini.

Uhuru ni hali ya kuwa na usismamizi binafsi katika mambo yako.Kama bado huwezi fanya maamuzi binafsi na kujitawala basi hauko huru.

Tumekuwa huru katika mambo mengi lakini hili limechelewa sana na limesababisha watu wengi kutokuendelea.

Jambo hilo ni UHURU WA KIFKRA .Mimi nasema ni afadhali utawaliwe kiuchumi ,kisiasa ,kitamaduuni n.k kuliko kutawaliwa kifkra.

Nchi nyingi zilitawaliwa lakini fikra za viongozi mfano Mwalimu Nyerere zililenga kufanya mageuzi ya kutoka katika  utawala huo kandamizi.

Mtu anayetawaliwa kifkra huongozwa kama remote katika mambo yake na huwa anategemea maamuzi  ya mtu au watu wengine.

Mtu huyu hawezi kujisimamia Mwenyewe yaani ni tegemezi  na mara nyingi mawazo yako hunyonywa na wakoloni (ndugu,jamaa na marafiki wenye mitazamo hasi).

Usipokuwa na uwezo wa kufanya mapinduzi ya kifkra na kutoka mikononi mwa tawala za watu wenye mitazamo hasi(wakoloni) ni wazi kuwa hautaweza kuendelea katika mambo yako mpaka unakufa.

Kuna wakati mwingine nchi zilitumia mtutu wa bunduki ili wawe huru toka vifungo vya kikoloni Vivyo hivyo unapaswa kufanya kila linalowezekana kujisimamia mwenyewe kimtazamo/kifkra na kuamua kutofuata mawazo hasi ya watu wasiotaka ufanikiwe

Joas (Jyb)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni