Jumamosi, Juni 04, 2016

“NGUVU YA LEO(The Power of Today)”




Mpendwa Naamini umzima !
Waswahili husema "samaki mkunje angali mbichi" na "udongo uwahi ungali maji.Mimi nataka nifaninanishe samaki na udongo kama wazo zuri la kibiashara ulililonalo wewe.
Mara nyingi Mungu amekuwa akawapa mawazo mazuri watu lakini huwa si watekelezaji(doers) wa mawazo haya kwa wakati na huwa huchukua Muda kutekeleza mawazo mazuri na pengine huwa mawazo yanakufa kabisa au mtu anatoweka (kufa) bila kuweka wazo lake kwenye utendaji .
Myles Mnuroe aliyekuwa mshauri wa kufikia mafanikio makubwa na Mhubiri wa Injili Wengi tutakuwa tunamfahamu (Nasikitika hatunaye sasa) alisema "When God see the Graves ,he wipes" akimanisha kuwa Mungu akiyatazama makaburi anasikitika kwa watu wamekufa na utajiri mkubwa vichwani mwao.
Ndugu yangu hakuna Muda mzuri kama sasa,waswahili husema “liwezekanalo leo,lisingoje kesho”.Msemo huu unamanisha kuwa kama una nguvu ya kufanya jambo leo lifanye tu kwa uwaredi maana kesho yako hauijui.Unaweza kusema nitafanya kesho ,kesho afya yako isiwe vizuri kulifanya.
Lameck Amos Hulilo Mkurugenzi wa Mpango Mkakati Technologies alitambua sili hii ya nguvu ya sasa/leo.Lameck kila alipopata wazo ,mara moja aliliweka katika utendaji.Kumbuka wazo la kwanza la Lameck ilikuwa kutengeneza Bussiness card akiwa chuo na aliliweka kwenye utendaji na akafanikiwa bila kusubiri eti mazingira yamsaidie.
Huna sababu ya kutoweka wazo lako kwenye uhalisia .Anneth Isaya Gerena ambaye tuliweza pata simulizi yake Kijana Jithamini watsap group  alilitambua hili japo ni Kiziwi .Anneth anasema "Mwaka 2010 January niliendelea kutafuta kazi bila mafanikio nilituma karibu application Mia lakini wapi.... February 2010 nikakaa chini na kutafakari, nikajisemea nguvu ninazo, elimu ninayo, maarifa ninayo, ujuzi ninao sasa kwa nini nihangaike kiasi hiki kutafuta kazi???? Nitatafuta mpaka lini?  Nitawategemea  wazazi na ndugu  hadi lini??????.Nikamuomba sana Mungu anipe ujasiri wa kufanya kitu katika maisha yangu kiwe suluhisho LA kuhangaika huko na kule kusaka kazi bila mafanikio..... Basi nikajikaza sikuwa na hata senti moja tuseme niite mtaji.Nikaamua kuwakusanya wanawake viziwi wenzangu ambao hawakuwa na elimu wala ajira kabisa mwenye Elimu nikiwa mimi pekee yangu... NikawAmbia mimi mwenzenu nimemaliza chuo lakini sijabahatika kupata kazi Lakini nina kitu nataka kuwafanyia ili kuwakomboa pamoja na kujikomboa mwenyewe.... Huo ndo ukawa mwanzo wa asasi ya furaha ya wanawake wajasirialiamali kwa viziwi Tanzania, FUWAVITA I am the founder and director of that NGO “
Wakati unasema huna mtaji Lameck Amos ambaye ni Mkurugenzi wa Mpango Mkakati Technologies hakuwa na Mtaji kama wewe leo anamiliki Kampuni yake , Francis Lutufyo Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Digital gates naye alianza hivo lakini pia Dada Anneth Isaya Gerana hakuwa na mtaji lakini yeye pia alikuwa mlemavu lakini alifanya kitu.Wewe uko fit asilimia 100% ,una mazingira mazuri, unasubiri nini???.

Nimalize kwa kusema ipo nguvu katika maamuzi magumu yako unayofanya sasa.AMUA KUFANYA KITU LEO:
  • Amua kuuza genge
  • Amua kuanzisha kampuni
  • Amua kuanzisha duka 
  • Amua kufanya mradi wowote 
  • Amua kutembeza nguo
  • Amua kupiga picha na kuziuza

AKUTAKIAYE KUFANIKIWA KATIKA MAISHA YAKO

Joas(Jyb)
0656110906


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni