Maisha ni safari ndefu naam katika
maisha yapo mengi tunayoona kwa macho yetu na tunayosikia kwa masikio yetu
.Yapo mengi ambayo tunakutana nayo katika maisha yetu ya kila siku .Kila jambo katika maisha halipo bure
lipo ili tuweze kijifunza kwalo na lijenge maisha yetu na kuyafanya kuwa bora
zaidi japo tumekuwa watu wa kupuuza kila aina ya maisha tunayopitia .

Unapokutana na mtu ambaye humjui mahali popote usimdharau maana humjui .Penda kujifunza kwa kila mtu unayekutana naye utashaangaa unajifunza mengi na pengine akawa chanzo cha maisha yako kubadilika na ukashangaa nini kimetokea .
Wakati tulipokuwa/tunapokuwa shuleni
,vyuoni ,makazini na kwingineko tunakutana na watu wenye malezi tofauti ,mawazo
tofauti ,hulka tofauti na tabia tofauti .Katika mazingira kama haya ni fursa
nzuri ya kujifunza mambo mengi na kuyachuja ili yakusaidie kuishi na kila mtu
hapa duniani .Watu wengi wanashindwa kuishi na watu kwa sababu wanashindwa
kujifunza kwa wale wanaokutana nao .
Zipo nyakati ambazo tunapita kwenye
shida kubwa na hulka ya binadamu ni kuwa hapendi apitie shida au
changamoto.Ushauri wangu ni kuwa unapokuw katika changamoto kubwa na shida
kubwa ni wakati wa kujifunza vitu vingi na kujenga msuli wa kuhimili kila gumu
unalopitia.Wakati wa magumu ni wakati ambapo akili na uwezo wa kufikiri hukua
kwa kiwango kikubwa sana .Ni wakati wa shida ni wakati ambao uwezo wwa kutatua
matatizo (problem solving capacity) inakuwa kubwa.
Upo pia wakati unafanikiwa na kuishi maisha ya ndoto
yako .Unapofanikiwa ni muda wa kukaa chini na kutafakari na kujifunza sana juu
ya maisha na kwanini wewe umefanikiwa na si mwingine .Si wakati wa kuwadharau
watu lakini ni wakati wako wa kumfundisha zaidi yule amabaye hajafikia maisha
yao .Jua kuwa pamoja na kuwa umefanikiwa kuna mahali ambapo ulipitia na wapo
watu waliopo mahali pale ulipopitia na wanahitaji msaada wako wa namna yoyote
ili nao watoke mahali walipo .
Joas (Jyb)0753836463/0656110906
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni